Tangazo la Shiwata created by innowise(Banners)



Wednesday, June 18, 2014

SHIWATA yagawa mashamba kwa wanachama wake

MTANDAO WA WASANII TANZANIA                 (SHIWATA)

          PRESS RELEASE

SHIWATA imeamua kutoa ofa ya kugawa shamba lake la ekari 500 lililoko Mkuranga mkoa wa Pwani kwa wanachama wake wenye uwezo wakulima mazao mbalimbali yatakayochangia kupunguza uhaba wa chakula nchini.

Taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa na Mwenyekiti wa Mtandao wa SHIWATA, Cassim Taalib kwa vyombo vya habari inasema wanachama watakaogaiwa shamba hilo ni wale walio hai walio lipia ada zao watapaswa kutoa sh. 200,000 kulipia ekari moja atakayopewa.

Alisema kuratibu mpango huo SHIWATA imeitisha mkutano wa wanachama wote Jumamosi Juni 21,2014 kwenye ukumbi wa Splendid Ilala ili kujadili mambo mbalimbali katika kijiji cha wasanii Mkuranga ambacho mpaka sasa kimejenga na kukabidhi nyumba 66 kwa wanachama wake kati ya 265 wanaojenga nyumba zao kwa njia ya kuchangishana.

"Ujenzi wa nyumba za kisasa katika kijiji chetu cha Mwanzega Mkuranga chenye ukubwa wa hekari 300 unaendelea tunatarajia kukabidhi nyumba 40 Desemba mwaka huu katika sherehe kubwa ambayo tunatarajia kumpata mgeni rasmi kutoka ngazi za juu" alisema Mwenyekiti.

Alisema shiwata inawataka wanachama wote ambao hawakuwahi kwenda kuona au kukabidhiwa viwanja au nyumba zao kutokana na sababu mbalimbali wafike na kadi zao ofisini Ilala Bungoni Chuo cha Splendid kabla ya Jumatano Juni 19, 2014 ili wakakabidhiwe nyumba zao na kiwanja vyao Jumamosi Juni 21, 2014 saa 2 asubuhi kwa nauli ya sh. 10,000 ya kwenda na kurudi.

Aliwatoa wasiwasi wanachama waliokuwa wanahofia kuwekeza katika ujenzi wa nyumba kuwa mpango wa kupimia wasanii nyumba zao ili wapate fursa ya kukopa kutoka benki mbalimbali za hapa nchini umeanza kushirikiana na Idara ya Ardhi ya Halmashauri ya Mkuranga ikifuatiwa na ujenzi wa barabara, uvutaji wa umeme na uchimbaji visima vya kisasa unafanyiwa kazi.

Aliwahimiza wanachama wanaochangia ujenzi wa nyumba zao kukamilisha michango hiyo ili wakabidhiwe nyumba zao kukamilisha malengo ya kuwasaidia wasanii kujikwamua kiuchumi.

Mtandao wa Wasanii Tanzania (SHIWATA) ulianzishwa mwaka 2004 na kusajiliwa na baraza la sanaa tanzania shiwata mwaka 2005 pia imesajiliwa na brella kwa shughuli za kiuchumi ikiwa na dira ya kuwakomboa wasanii kuwa na maisha bora kupitia mtandao huu ifikapo mwaka 2015.

Kwa maelezo zaidi wasiliana na Ofisa Habari wa SHIWATA, Peter Mwenda 0715/0752 222677.

mwisho.

No comments:

Post a Comment

Advertising Here