Zoezi la ukaguzi wa Stempu kwenye bidhaa za Filamu latikisa Dar
Mjumbe
wa Kamati ya Urasimishaji wa Kazi za wasanii wa Filamu na Muziki hapa
nchini ambaye pia ni Afisa kutoka Bodi ya Filamu Tanzania Bw. Wilhad
Tairo akifafanua jambo kwa mfanyabiashara wa duka la Filamu wakati wa
Operesheni ya kukagua Bidhaa zisizo kuwa na Stempu za TRA, Operesheni
hiyo ya wiki mbili iliyoanza jana jijini Dar es Salaaminatekelezwa kwa
uhirikiano wa TRA, Bodi ya Filamu, Basata na Cosota
Mfanyabiashara wa duka CDs za Filamu lililopo maeneo ya Kariakoo jijini Dar es Salaam akieleza jambo kwa maafisa wa Kikosi kazi kwa ajili yakukagua bidhaa ambazo azizingatii taratibu kabla ya kuingizwa sokoni leo jijini Dar es Salaam.
Muuzaji wa duka la CD za Filamu katika mitaa ya Kariakoo jijini Dar es Salaam akiwaonyesha Stempu za TRA katika CD zake wakaguzi kutoka TRA,Bodi ya Fila, Basata na Costa ambao walifika dukani kwake kwa ajili ya ukaguzi wa bidhaa ambazo zimeingizwa sokoni bila kufuata taratibu za kisheria iliwemo kuweka Stika za TRA kama sheria inavyotaka.Kamati ya urasimishaji wa kazi za wasanii wa Filamu na Muziki wameanza Operesheni ya wiki mbili katika jiji la Dar es Salaam ili kuleta ufanisi katika mapato ya Wasanii.
Afisa Kodi Msaidizi Bi. Theophilda Majara( Mwenye blauzi nyekundu) akikagua baadhi ya CD za Filamu wakati wa Operesheni ya kukagua Filamu ambazo hazijafuata taratibu za kisheria ikiwemo kulipia Stempu ya TRA kabla ya kuingia sokoni. Zoezi hilo linaendeshwa kwa ushirikiano wa TRA, Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo kupitia Bodi ya Filamu, Basata na Costota .
Baadhi ya wananchi wakifuatilia namna Operesheni ya kukagua Filamu zilizoingia sokoni bila kufuata utaratibu namna inavyotelekelezwa jana katika mitaa ya Kariakoo jijini Dar es Salaam.
Mfanyabiashara wa duka CDs za Filamu lililopo maeneo ya Kariakoo jijini Dar es Salaam akieleza jambo kwa maafisa wa Kikosi kazi kwa ajili yakukagua bidhaa ambazo azizingatii taratibu kabla ya kuingizwa sokoni leo jijini Dar es Salaam.
Muuzaji wa duka la CD za Filamu katika mitaa ya Kariakoo jijini Dar es Salaam akiwaonyesha Stempu za TRA katika CD zake wakaguzi kutoka TRA,Bodi ya Fila, Basata na Costa ambao walifika dukani kwake kwa ajili ya ukaguzi wa bidhaa ambazo zimeingizwa sokoni bila kufuata taratibu za kisheria iliwemo kuweka Stika za TRA kama sheria inavyotaka.Kamati ya urasimishaji wa kazi za wasanii wa Filamu na Muziki wameanza Operesheni ya wiki mbili katika jiji la Dar es Salaam ili kuleta ufanisi katika mapato ya Wasanii.
Afisa Kodi Msaidizi Bi. Theophilda Majara( Mwenye blauzi nyekundu) akikagua baadhi ya CD za Filamu wakati wa Operesheni ya kukagua Filamu ambazo hazijafuata taratibu za kisheria ikiwemo kulipia Stempu ya TRA kabla ya kuingia sokoni. Zoezi hilo linaendeshwa kwa ushirikiano wa TRA, Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo kupitia Bodi ya Filamu, Basata na Costota .
Baadhi ya wananchi wakifuatilia namna Operesheni ya kukagua Filamu zilizoingia sokoni bila kufuata utaratibu namna inavyotelekelezwa jana katika mitaa ya Kariakoo jijini Dar es Salaam.
Picha na Frank Shija- Afisa Mawasiliano Serikalini,
Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo
Tuesday, May 27, 2014
KUMBUKUMBU YA KIFO CHA MANGWEA JUNI 28, MOROGORO
..Mastaa kibao kujumuika katika ‘Love concert’
..Afande Selle, Belle 9, Samir na wengineo,Moro
MASTAA mbalimbali nchini wakiwemo wanamuziki wanatarajiwa kushiriki kwenye tukio maalum la kumbukumbu ya mwaka mmoja tokea kifo cha marehemu Albert Mangwea ‘Ngwair’ , litakalofanyika ndani ya ukumbi wa Nyumbani Park (Samaki samaki Spot) , Kihonda Morogoro mjini Juni 28.
Akizungumza na mtando huu , Mratibu Mtendaji wa tamasha hilo, Kareeem Omary ‘KO’ alisema maandalizi ya tukio hilo litakalokuwa la kila mwaka, limepwa jina la ‘Love Concert - Kumbukumbu ya kifo cha Albert Mangwe’.
Kareem, aliwaomba wadau kujitokeza kwa wingi kuunga mkono kwenye tukio hilo kwani litakuwa la kipekee na la aina yake ambalo pia litatoa fursa kwa wakazi hao pia mikoa jirani na watu kutoka nje ya Tannzania ambao watauzulia.
“Nawaomba wadau kujitokeza kuonesha upendo wa pamoja. Kumbukumbu kwa mpendwa wetu kama ilivyo utamaduni wetu.” alisema Kareem.
Na kuongeza kuwa, siku hiyo Watu mbalimbali watapata kupiga picha na mastaa pamoja na mama mzazi wa Mangwea kama kumbukumbu.
Kareem aliwataja wasanii watakaotoa burundani, ni pamoja na kutoka kwa kundi la Wanachemba ambalo pia aliwahi kuwa nalo marehemu Ngwair, JSqueezer, P Funky Majani na Mswaki. Kwa upande wa wasanii kutoka Morogoro ni pamoja na Afande Sele, Team Racers, Mc Koba Chris wa Marya, Belle 9, Samir, Zombie, President Mirrow, Jordan wa Dejavu na wengine wengi.
Katika siku hiyo ya Juni 28, ambayo ndiyo siku aliyopatwa na umati marehemu, Kareem alisema kabla ya matukio ya shoo ukumbini, itatanguliwa na ibada mbili maalum ikiwemo ya Kanisani na ile ya nyumbani.
Aidha, Kareem alisema katika tukio hilo, ambalo linatarajia kuanza majira ya jioni ya saa 10 hadi saa 12 jioni, wametoa fursa kwa watoto kutoa burudani ikiwemo ya kuimba na nyinginezo na baadae usiku wa kuanzia saa 2 hadi majogoo wasanii hao mbalimbali watatawala jukwaa na burudani ya nguvu ya kumbukumbu.
Marehemu ‘Ngwair’ alifariki dunia akiwa nchini Afrika kusini, alijizolea umaarufu kwa nyimbo kama Mikasi na Nisikilize Mi na nyingine nyingi alizowahi shirikishwa na wasanii mbalimbali nchini wakiwemo Professa Jay, Nuru, TID, Chidi Benz na wengine wengi.
mwisho
No comments:
Post a Comment